Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake.
Utukufu wake ni mkuu kwa wokovu wako, Heshima na adhama waweka juu yake.
Wewe U mwenye fahari na adhama, Toka milima ya mateka.
Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako, Na adhama yako kwa watoto wao.
Heshima na adhama ziko mbele zake, Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Wewe, Bwana, Mungu wangu, Umejifanya mkuu sana; Umejivika heshima na adhama.
Kazi yake ni heshima na adhama, Na haki yake yakaa milele.
Lakini tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu.