Bwana akamsikia Hezekia, akawaponya watu.
Walilia, naye Bwana akasikia, Akawaponya na taabu zao zote.
Na habari zake zikaenea katika Shamu yote; wakamletea wote waliokuwa hawawezi, walioshikwa na maradhi mbalimbali na mateso, wenye pepo, na wenye kifafa, na wenye kupooza; akawaponya.
Naye Yesu hali akiyafahamu hayo akaondoka huko; na watu wengi wakamfuata; akawaponya wote,
Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.
Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya;
Makutano mengi wakamfuata, akawaponya huko.
Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya.
Wala hakuweza kufanya mwujiza wo wote huko, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya.
Na makutano walipojua walimfuata; akawakaribisha, akawa akisema nao habari za ufalme wa Mungu, akawaponya wale wenye haja ya kuponywa.