Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.
Kwa sababu hiyo jina lake likaitwa Babeli; maana hapo ndipo Bwana alipoichafua lugha ya dunia yote; na kutoka huko Bwana akawatawanya waende usoni pa nchi yote.
Akapiga mishale, akawatawanya; Umeme, naye akawatapanya.
Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.