Basi hii ndiyo misingi ya majengo ya nyumba ya Mungu aliyoiweka Sulemani. Urefu wake kwa mikono ya cheo cha kwanza ulikuwa mikono sitini, na upana wake mikono ishirini.
Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea Bwana kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.
Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.