Na mtu awaye yote akifanya dhambi, kwa kuwa ameisikia sauti yenye kuapisha, naye akawa ni shahidi, kwamba aliona au kujua, asipolifunua neno lile, ndipo atakapochukua uovu wake mwenyewe;
Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu; Kwa kuwa Bwana ameisikia sauti ya kilio changu.
Bwana ameisikia dua yangu; Bwana atayatakabali maombi yangu.
Na ahimidiwe Bwana. Maana ameisikia sauti ya dua yangu;