Maana huwi Mungu apendezwaye na ubaya; Mtu mwovu hatakaa kwako;
Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema?
Washangilie na kufurahi, Wapendezwao na haki yangu. Naam, waseme daima, Atukuzwe Bwana, Apendezwaye na amani ya mtumishi wake.
Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.