Maana atakapokufa hatachukua cho chote; Utukufu wake hautashuka ukimfuata.
Mtu mwovu atakapokufa, taraja lake lapotea; Na matumaini ya uovu huangamia.
bali katika mahali pale walipomchukua mateka ndipo atakapokufa, wala hataiona nchi hii tena kamwe.
Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika mahali pale akaapo mfalme aliyemmilikisha, ambaye alikidharau kiapo chake, na kulivunja agano lake, ndipo atakapokufa pamoja naye kati ya Babeli.