Watumwa wake wakamwambia, Angalia sasa, tumesikia ya kuwa wafalme wa nyumba ya Israeli ni wafalme wenye rehema; tafadhali, tuvae magunia viunoni, na kamba vichwani, tumtokee mfalme wa Israeli; labda atakuokoa roho yako.
Yeye atakuokoa na mateso sita; Naam, hata katika saba hapana uovu utakaokugusa.
Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji, Na katika tauni iharibuyo.
Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa.