Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako.
Nawachukia kwa ukomo wa chuki, Wamekuwa adui kwangu.
Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake.
Ingawa chuki hufunikizwa kwa hila; Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko.
Na kwa ajili ya hayo yote, nikatia moyo wangu katika kuyatafuta-tafuta haya; ya kuwa wenye haki, na wenye hekima, pamoja na matendo yao yote, wamo mkononi mwa Mungu; kwamba ni pendo au kwamba ni chuki, mwanadamu hajui; mambo yote yawapita.
nao watakutenda mambo kwa chuki, watakuondolea kazi zako zote, watakuacha uchi, huna nguo na aibu ya mambo yako ya kikahaba itafunuliwa, uasherati wako na uzinzi wako.