Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki.
Lakini mimi ningemtafuta Mungu, Ningemwekea Mungu daawa yangu;
Ningeiweka daawa yangu mbele yake, Na kukijaza kinywa changu hoja.
Nalikuwa baba kwa mhitaji, Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza.
Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;