Ili wazishike amri zake, na kuzitii sheria zake. Haleluya.
Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.
Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana.
Haleluya. Israeli alipotoka Misri, Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.
Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote, mhimidini.
Haleluya. Lisifuni jina la Bwana, Enyi watumishi wa Bwana, sifuni.
Na ahimidiwe Bwana toka Sayuni, Akaaye Yerusalemu. Haleluya.
Bwana atamiliki milele, Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi. Haleluya.
Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri.
Hakulitendea taifa lo lote mambo kama hayo, Wala hukumu zake hawakuzijua. Haleluya.
Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.
Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.
Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.