Daudi akaapa, akasema, Baba yako anajua sana ya kuwa nimeona kibali machoni pako, naye asema, Yonathani asilijue neno hili, asije akahuzunika; lakini ni kweli, aishivyo Bwana, na iishivyo roho yako, iko hatua moja tu kati ya mimi na mauti.
Hata ikawa, watu waliolichukua sanduku la Bwana walipokwisha kwenda hatua sita, akachinja ng'ombe na kinono.
Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Wala miguu yangu haikuteleza.
Mguu wangu umeshikamana sana na hatua zake; Njia yake nimeishika, wala sikukengeuka.
Wakati hatua zangu zilipokuwa zikioshwa kwa siagi, Nalo jabali liliponimiminia mito ya mafuta!
Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?
Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
Ningemwambia hesabu ya hatua zangu Ningemkaribia kama vile mkuu.
Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Na miguu yangu haikuteleza.
Hatua za mtu zaimarishwa na Bwana, Naye aipenda njia yake.
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake. Hatua zake hazitelezi.
Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.
Nami miguu yangu ilikuwa karibu na kupotoka, Hatua zangu zilikuwa karibu na kuteleza.
Haki itakwenda mbele zake, Nayo itazifanya hatua zake kuwa njia.
Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi
Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, Uovu usije ukanimiliki.
Miguu yake inatelemkia mauti; Hatua zake zinashikamana na kuzimu;
Moyo wa mtu huifikiri njia yake; Bali Bwana huziongoza hatua zake.
Siti msharifu, jinsi zilivyo nzuri Hatua zako katika mitalawanda. Mapaja yako ya mviringo ni kama johari, Kazi ya mikono ya fundi mstadi;
Bwana akasema tena, Kwa sababu binti za Sayuni wana kiburi, na kuenenda na shingo zilizonyoshwa, na macho ya kutamani, wakienenda kwa hatua za madaha, na kuliza njuga kwa miguu yao;
Mguu utaukanyaga chini, Naam, miguu yao walio maskini, Na hatua zao walio wahitaji.
Ee Bwana, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.