Skip to Content

"henoko"

11 mara katika SUV

Kaini akamjua mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Henoko; akajenga mji akauita Henoko, kwa jina la mwanawe.

Henoko akamzaa Iradi, Iradi akamzaa Mehuyaeli; Mehuyaeli akamzaa Methushaeli; Methushaeli akamzaa Lameki.

Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko.

Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.

Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela.

Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake.

Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano.

Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.

na Henoko, na Methusela, na Lameki;

Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.

Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,