Mizizi yake huzonga-zonga chuguu, Huangalia mahali penye mawe.
Mjinga huamini kila neno; Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.
Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
Huangalia sana njia za watu wa nyumbani mwake; Wala hali chakula cha uvivu.
Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu, Aliye juu kuliko walio juu huangalia; Tena wako walio juu kupita hao.
Naam, koikoi angani ajua nyakati zake zilizoamriwa; na hua na mbayuwayu na korongo huangalia wakati wa kuja kwao; bali watu wangu hawazijui amri za Bwana.