Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.
Ndugu zote wa maskini humchukia; Jinsi gani rafiki zake huzidi kujitenga naye! Huwafuata kwa maneno, lakini wametoweka.
Wamwagao damu humchukia mtu mkamilifu; Bali wenye haki humtunza nafsi yake.
Wao humchukia yeye akemeaye langoni, nao humzira anenaye maneno ya adili.
Yeye anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu.