Skip to Content

"husuda"

13 mara katika SUV

Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa.

Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;

Mwenye husuda afanya haraka kuwa tajiri; Wala haufikiri uhitaji utakaomjilia.

Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote lililofanyika chini ya jua.

Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.

Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa husuda.

Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,

kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?

husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.

Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.

amejivuna; wala hafahamu neno lo lote; bali ana wazimu wa kuwazia habari za maswali, na mashindano ya maneno, ambayo katika hayo hutoka husuda, na ugomvi, na matukano, na shuku mbaya;

Maana hapo zamani sisi nasi tulikuwa hatuna akili, tulikuwa waasi, tumedanganywa, huku tukitumikia tamaa na anasa za namna nyingi, tukiishi katika uovu na husuda, tukichukiza na kuchukiana.

Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.