Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa Bwana hutafuta-tafuta mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, ataonekana nawe; ukimwacha, atakutupa milele.
Upana wa milima ni malisho yake, Hutafuta-tafuta kila kitu kilicho kibichi.
Atafutaye mema kwa bidii hutafuta fadhili; Atafutaye madhara, hayo yatamjia.
Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate; Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.
Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.
Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
Watu wengi hutafuta upendeleo wa mkuu; Bali hukumu ya kila mtu hutoka kwa Bwana
Hutafuta sufu na kitani; Hufanya kazi yake ya mikono kwa moyo.
Yeye anenaye kwa nafsi yake tu hutafuta utukufu wake mwenyewe; bali yeye anayetafuta utukufu wake aliyempeleka, huyo ni wa kweli, wala ndani yake hamna udhalimu.