Maana mioyo yetu itamfurahia, Kwa kuwa tumelitumainia jina lake takatifu.
Na nafsi yangu itamfurahia Bwana, Na kuushangilia wokovu wake.
Na watu wa Efraimu watakuwa kama shujaa, na moyo wao utafurahi kana kwamba ni kwa divai; naam, watoto wao wataona mambo haya, na kufurahi; mioyo yao itamfurahia Bwana.