Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi, Na giza tupu li katika kope zangu;
Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi, Wala kope zangu kusinzia;
Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana.
na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji.