akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi.
na kila kunguru kwa aina zake;
na kila kunguru kwa aina zake;
Itakuwa utakunywa maji ya kile kijito; nami nimewaamuru kunguru wakulishe huko.
Kunguru wakamletea mkate na nyama asubuhi, na mkate na nyama jioni, akanywa maji ya kile kijito.
Humpa mnyama chakula chake, Wana-kunguru waliao.
Jicho la mtu amdhihakiye babaye, Na kudharau kumtii mamaye; Kunguru wa bondeni wataling'oa, Na vifaranga vya tai watalila.
Kaati na nungu wataimiliki, bundi na kunguru watakaa huko, naye atanyosha juu yake kamba ya ukiwa na timazi ya utupu.
Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!