Uniongoze katika kweli yako, Na kunifundisha. Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu, Nakungoja Wewe mchana kutwa.
Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako.
Umwangazie mtumishi wako uso wako, Na kunifundisha amri zako.