Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.
Ee Bwana, uyasikilize maneno yangu, Ukuangalie kutafakari kwangu.
Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake.
Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Mimi nitamfurahia Bwana.
Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.
Paulo akasimama katikati ya Areopago, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.