Lakini mimi ni mdudu wala si mtu, Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu.
Kwa sababu ya watesi wangu nimekuwa laumu, Naam, hasa kwa jirani zangu; Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu; Walioniona njiani walinikimbia.
Uniokoe na maasi yangu yote, Usinifanye laumu ya mpumbavu.
Maana kwa ajili yako nimestahimili laumu, Fedheha imenifunika uso wangu.
Maana wivu wa nyumba yako umenila, Na laumu zao wanaokulaumu zimenipata.
Nilipolia na kuiadhibu roho yangu kwa kufunga, Ikawa laumu juu yangu.
Laumu imenivunja moyo, Nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna; Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.
Uwalipe jirani zetu mara saba vifuani mwao Laumu zao walizokulaumu, Ee Bwana.
Wote wapitao njiani wanateka mali zake; Amekuwa laumu kwa jirani zake;
Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema.
Heri kusikia laumu ya wenye hekima, Kuliko mtu kusikia wimbo wa wapumbavu;
watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.