Skip to Content

"mapato"

12 mara katika SUV

Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi;

Isipokuwa wanyama wa mji na nyara za mji Israeli wakatwaa wenyewe kuwa ni mapato yao, sawasawa na hilo neno la Bwana alilomwamuru Yoshua.

Na mfalme alipomwuliza yule mwanamke, yeye akamweleza. Basi mfalme akamtolea akida, akasema, Mrudishie yote aliyokuwa nayo, na mapato yote ya shamba lake tangu siku aliposafiri, hata leo.

Afadhali mali kidogo pamoja na haki, Kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.

Yeye awaoneaye maskini ili kuongeza mapato, Naye ampaye tajiri, hupata hasara.

Moyo wa mumewe humwamini, Wala hatakosa kupata mapato.

Huangalia shamba, akalinunua; Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

Mpe mapato ya mikono yake, Na matendo yake yamsifu malangoni.

Na biashara yake na ujira wake utakuwa wakfu kwa Bwana, hautawekwa hazinani wala hautawekwa akiba; bali mapato ya biashara yake yatakuwa mali zao wakaao mbele za Bwana, wapate kula na kushiba, na kuvaa mavazi ya fahari.

Mimi nafunga mara mbili kwa juma; hutoa zaka katika mapato yangu yote.

Maana adhulumuye atapata mapato ya udhalimu wake, wala hakuna upendeleo.

Hao wanapindua watu wa nyumba nzima, wakifundisha yasiyowapasa kwa ajili ya mapato ya aibu.