Skip to Content

"mapito"

26 mara katika SUV

Yeye ameiziba njia yangu nisipate kupita, Na kutia giza katika mapito yangu.

Hawa ni katika hao waliouasi mwanga; Hawazijui njia zake, Wala hawakai katika mapito yake.

Hunitia miguu yangu katika mkatale, Na mapito yangu yote huyapeleleza.

Hufanya mapito yake kung'aa nyuma yake Hata mtu angedhani kilindi kina mvi.

Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,

Umeuvika mwaka taji ya wema wako; Mapito yako yadondoza unono.

Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, Kwa maana nimependezwa nayo.

Nilipozimia roho uliyajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.

Mwanangu, usiende njiani pamoja nao; Uzuie mguu wako usiende katika mapito yao.

Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.

Waliopotoka katika njia zao; Walio wakaidi katika mapito yao.

Maana nyumba yake inaelekea mauti, Na mapito yake yanakwenda kwenye wafu.

Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki.

Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.

Njia zake ni njia za kupendeza sana, Na mapito yake yote ni amani.

Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.

Natembea katika njia ya haki, Katikati ya mapito ya hukumu.

Katika njia ya haki kuna uhai; Wala hakuna mauti katika mapito yake.

Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu.

Katika habari za watu wangu, watoto ndio wanaowaonea, na wanawake ndio wanaowatawala. Enyi watu wangu, wakuongozao wakukosesha, waiharibu njia ya mapito yako.

tokeni katika njia, geukeni mtoke katika mapito; mkomesheni Mtakatifu wa Israeli mbele yetu.

Nitawaleta vipofu kwa njia wasiyoijua; katika mapito wasiyoyajua nitawaongoza; nitafanya giza kuwa nuru mbele yao; na mahali palipopotoka kuwa pamenyoka. Haya nitayatenda, wala sitawaacha.

Maana watu wangu wamenisahau, wameufukizia ubatili uvumba; nao wamewakaza katika njia zao, katika mapito ya zamani, ili wapite katika njia za kando, katika njia isiyotengenezwa;

Basi kwa ajili ya hayo, angalia, nitaiziba njia yako kwa miiba, nami nitafanya kitalu juu yake, asipate kuyaona mapito yake.

Kwa sababu huyo ndiye aliyenenwa na nabii Isaya, akisema, Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.

Sauti ya mtu aliaye nyikani, Itengenezeni njia ya Bwana, Yanyosheni mapito yake.