Skip to Content

"mausia"

31 mara katika SUV

Kwa ajili ya hayo yashikeni mausia yangu, ili kwamba msifanye kabisa desturi hizi zichukizazo mojawapo, zilizotangulia kufanywa mbele zenu, wala msijitie unajisi katika mambo hayo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.

Basi kwa hiyo watayashika mausia yangu, wasije wakachukua dhambi kwa hayo, nao wakafa humo, wakiyanajisi; mimi ndimi Bwana niwatakasaye.

Na mausia ya mzigo wao ni haya, kwa utumishi wao wote katika hema ya kukutania; mbao za maskani, na mataruma yake, na nguzo zake, na matako yake;

Kwa ajili hii mpende Bwana, Mungu wako, na kushika sikuzote mausia yake, na amri zake, na hukumu zake, na maagizo yake.

hamkuwaacha hao ndugu zenu siku hizi nyingi hata hivi leo, lakini mmeyashika mausia ya amri ya Bwana, Mungu wenu.

uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako;

Nawe ukienda katika njia zangu, na kuyashika mausia yangu, na amri zangu, kama baba yako Daudi alivyokwenda, basi nitazifanya siku zako kuwa nyingi.

Wewe umetuamuru mausia yako, Ili sisi tuyatii sana.

Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako.

Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.

Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.

Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.

Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.

Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.

Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.

Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.

Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, Lakini sikuyaacha mausia yako.

Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.

Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.

Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu.

Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.

Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.

Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.

Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu, Nipate kuyashika mausia yako.

Mimi ni mdogo, nadharauliwa, Lakini siyasahau mausia yako.

Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na fadhili zako.

Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.

Midomo yangu na itoe sifa, Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.

Mkono wako na uwe tayari kunisaidia, Maana nimeyachagua mausia yako.

Maneno ya Aguri bin Yake; mausia mtu huyu aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.

Maneno ya mfalme Lemueli; mausia aliyofundishwa na mama yake.