Ninyi mnaomcha Bwana, msifuni, Enyi nyote mlio wazao wa Yakobo, mtukuzeni, Mcheni, enyi nyote mlio wazao wa Israeli.
Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni Bwana, Enyi watu wote, mhimidini.
Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema, Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza.
Haleluya. Msifuni Bwana; Maana ni vema kumwimbia Mungu wetu, Maana kwapendeza, kusifu ni kuzuri.
Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.