Skip to Content

"mwimbieni"

19 mara katika SUV

Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.

Mwimbieni Bwana, nchi yote; Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.

Mwimbieni Bwana akaaye Sayuni, Yatangazeni kati ya watu matendo yake.

Mwimbieni Bwana zaburi, Enyi watauwa wake. Na kufanya shukrani. Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

Mshukuruni Bwana kwa kinubi, Kwa kinanda cha nyuzi kumi mwimbieni sifa.

Mwimbieni wimbo mpya, Pigeni kwa ustadi kwa sauti ya shangwe.

Mwimbieni Mungu, naam, imbeni; Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.

Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.

Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.

Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Mwimbieni Bwana, nchi yote.

Mwimbieni Bwana, libarikini jina lake, Tangazeni wokovu wake siku kwa siku.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Kwa maana ametenda mambo ya ajabu. Mkono wa kuume wake mwenyewe, Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.

Mwimbieni Bwana zaburi kwa kinubi, Kwa kinubi na sauti ya zaburi.

Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote.

Mwimbieni Bwana kwa kushukuru, Mwimbieni Mungu wetu kwa kinubi.

Haleluya. Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.

Mwimbieni Bwana; kwa kuwa ametenda makuu; Na yajulikane haya katika dunia yote.

Mwimbieni Bwana wimbo mpya, Na sifa zake tokea mwisho wa dunia; Ninyi mshukao baharini, na vyote vilivyomo, Na visiwa, nao wakaao humo.