Nikajifanyizia kazi zilizo kubwa; nikajijengea nyumba; nikajipandia mashamba ya mizabibu;
nikajifanyizia bustani na viunga, na kuipanda humo miti yenye matunda ya kila namna;
nikajifanyizia birika za maji, ya kuunyweshea mwitu mlimopandwa miti michanga.