upate kumcha Bwana, Mungu wako, kushika amri zake zote, na sheria zake, ninazokuamuru, wewe na mwanao, na mwana wa mwanao, siku zote za maisha yako; tena siku zako ziongezwe.
Basi zishike amri, na sheria, na hukumu ninazokuamuru leo, uzitende.
Jihadhari, usije ukamsahau Bwana, Mungu wako, kwa kutozishika amri zake, na hukumu zake, na sheria zake, ninazokuamuru leo.
kuzishika amri za Bwana na sheria zake, ninazokuamuru leo, upate uheri?