Ee Mungu wangu, Nimekutumaini Wewe, nisiaibike, Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.
Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe.
Nimekukimbilia Wewe, Bwana, Nisiaibike milele. Kwa haki yako uniponye,
Na waaibike watu wanaoniudhi, lakini nisiaibike mimi; na waone hofu kuu, lakini mimi nisione hofu kuu; ulete juu yao siku ya uovu; uwaangamize maangamizo maradufu.