Ee nguvu zangu, nitakuimbia kwa furaha, Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu, Mungu wa fadhili zangu.
Rehema na hukumu nitaziimba, Ee Bwana, nitakuimbia zaburi.
Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu, Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.
Nitakushukuru kwa moyo wangu wote, Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, Kwa kinanda chenye nyuzi kumi nitakuimbia.