Akaondoka huko akachimba kisima kingine, wala hicho hawakukigombania. Akakiita jina lake Rehobothi, akasema, Kwa kuwa sasa Bwana ametufanyia nafasi, nasi tutazidi katika nchi.
Samla akafa, naye Shauli, wa Rehobothi karibu na Mto, akamiliki badala yake.