Skip to Content

"reueli"

5 mara katika SUV

Walipofika kwa Reueli baba yao, akasema, Imekuwaje hata mkarejea mapema leo?

Kisha Musa akamwambia Hobabu, mwana wa Reueli Mmidiani, mkwewe Musa, Sisi twasafiri kwenenda mahali ambapo Bwana amenena habari zake hivi, Nitawapa ninyi mahali hapo; uje pamoja nasi, nasi tutakufanyia mema; kwa kuwa Bwana ametamka mema juu ya Israeli.

Wana wa Esau; Elifazi, na Reueli, na Yeushi, na Yalamu, na Kora.

Wana wa Reueli; Nahathi, na Zera, na Shama, na Miza.

na Ibneya, mwana wa Yerohamu; na Ela, mwana wa Uzi, mwana wa Mikri; na Meshulamu, mwana wa Shefatia, mwana wa Reueli, mwana wa Ibniya;