Ila Yonathani hakusikia, hapo babaye alipowaagiza watu kwa kiapo; basi yeye akainyosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake, na kuichovya katika sega la asali, kisha akatia mkono wake kinywani; na macho yake yakatiwa nuru.
Maneno yapendezayo ni kama sega la asali; Ni tamu nafsini, na afya mifupani.
Mwanangu, ule asali, kwa maana ni njema, Na sega la asali lililo tamu ulionjapo.