Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?
Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?
Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?
Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?