Basi sasa, tafadhali, wewe uisikilize sauti ya mjakazi wako, nikakuandalie ngaa mkate kidogo; ukale, ili upate nguvu, utakapokwenda zako.
Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo.
Ee Mungu, uisikilize sala yangu, Wala usijifiche nikuombapo rehema.
Ee Bwana, uyasikie maombi yangu; Uisikilize sauti ya dua zangu.