Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Umenifanyizia nafasi wakati wa shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.
Bwana, unifadhili, maana ninanyauka; Bwana, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.
Wewe, Bwana, unifadhili, Tazama mateso niteswayo na wanaonichukia; Wewe uniinuaye katika malango ya mauti,
Ee Bwana, usikie, kwa sauti yangu ninalia, Unifadhili, unijibu.
Ee Bwana, unifadhili, maana ni katika dhiki, Jicho langu limenyauka kwa masumbufu, Naam, mwili wangu na nafsi yangu.
Nami nalisema, Bwana, unifadhili, Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.
Lakini Wewe, Bwana, unifadhili, Uniinue nipate kuwalipa.
Wewe, Bwana, unifadhili, Maana nakulilia Wewe mchana kutwa.
Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, Unifadhili sawasawa na ahadi yako.