Ee Bwana, unijulishe njia zako, Unifundishe mapito yako,
Ee Bwana, unifundishe njia yako, Na kuniongoza katika njia iliyonyoka; Kwa sababu yao wanaoniotea;
Ee Bwana, unifundishe njia yako; Nitakwenda katika kweli yako; Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;
Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.
Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako.
Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hata mwisho.
Bwana, dunia imejaa fadhili zako, Unifundishe amri zako.
Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako.
Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.
Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe.
Unifundishe kuyatenda mapenzi yako, Kwa maana ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema aniongoze kwenye nchi sawa,