Skip to Content

"unihuishe"

10 mara katika SUV

Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako.

Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako.

Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.

Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.

Nimeteswa mno; Ee Bwana, unihuishe sawasawa na neno lako.

Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na hukumu yako.

Unitetee na kunikomboa, Unihuishe sawasawa na ahadi yako.

Ee Bwana, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na hukumu zako.

Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na fadhili zako.

Ee Bwana, unihuishe kwa ajili ya jina lako, Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;