Skip to Content

"uniokoe"

17 mara katika SUV

Uniokoe sasa na mkono wa ndugu yangu, mkono wa Esau, maana mimi namwogopa, asije akanipiga, na mama pamoja na wana.

Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.

Bwana urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

Kinywani mwa simba uniokoe; Naam, toka pembe za nyati umenijibu.

Unitegee sikio lako, uniokoe hima. Uwe kwangu mwamba wa nguvu, Nyumba yenye maboma ya kuniokoa.

Umwangaze mtumishi wako Kwa nuru ya uso wako; Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

Uniokoe na maasi yangu yote, Usinifanye laumu ya mpumbavu.

Ee Mungu, kwa jina lako uniokoe, Na kwa uweza wako unifanyie hukumu.

Uniponye nao wafanyao maovu, Uniokoe na watu wa damu.

Ee Mungu, uniokoe, Maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu.

Ee Mungu, uniokoe, Ee Bwana, unisaidie hima.

Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.

Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.

Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, Maana sikuisahau sheria yako.

na kwa sehemu iliyobakia hufanya mungu, yaani, sanamu yake ya kuchonga; husujudu mbele yake akaiabudu, akaiomba, akasema, Uniokoe; maana wewe u mungu wangu.

Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.

Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii.