Basi sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja nami, nipate kumwabudu Bwana.
Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, Unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.
Utazame teso langu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote.
Wakaanza wote kutoa udhuru kwa nia moja. Wa kwanza alimwambia, Nimenunua shamba, sharti niende nikalitazame; tafadhali unisamehe.
Mwingine akasema, Nimenunua ng'ombe jozi tano, ninakwenda kuwajaribu; tafadhali unisamehe.