Mfalme wa Sodoma, na mfalme wa Gomora, na mfalme wa Adma, na mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari, wakatoka wakapanga vita panapo bonde la Sidimu;
Wakafikilia Elimu, palipokuwa na chemchemi kumi na mbili, na mitende sabini; wakapanga hapo, karibu na maji.
Wakasafiri kutoka Makelothi, wakapanga Tahathi.
Baada ya hayo watu wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga kambi katika nyika ya Parani.
Kisha wana wa Israeli wakasafiri, wakapanga marago Obothi.
Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika jangwa iliyoelekea Moabu, upande wa maawio ya jua.
Kutoka huko wakasafiri, wakapanga katika bonde la Zeredi.
Kutoka huko wakasafiri, wakapanga upande wa pili wa Arnoni, ulio jangwani, utokao katika mpaka wa Waamori; maana, Arnoni ndio mpaka wa Moabu, kati ya Moabu na Waamori.
Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi, wakapanga katika Sukothi.
Kisha wakasafiri kutoka Sukothi, wakapanga Ethamu, palipo katika mwisho wa nyika.
Wakasafiri kutoka Ethamu, na kurudi nyuma hata Pi-hahirothi palipokabili Baal-sefoni; wakapanga mbele ya Migdoli.
Wakasafiri kutoka hapo mbele ya Hahirothi, wakapita katikati ya bahari na kuingia jangwani; kisha wakaenda safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu, wakapanga Mara.
Wakasafiri kutoka Mara, wakafikilia Elimu; huko Elimu palikuwa na chemchemi za maji kumi na mbili, na mitende sabini; nao wakapanga hapo.
Wakasafiri kutoka Elimu wakapanga karibu na Bahari ya Shamu.
Wakasafiri kutoka Bahari ya Shamu, wakapanga katika nyika ya Sini.
Wakasafiri kutoka nyika ya Sini, wakapanga Dofka.
Wakasafiri kutoka Dofka, wakapanga Alushi.
Wakasafiri kutoka Alushi, wakapanga Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya watu kunywa.
Wakasafiri kutoka Refidimu, wakapanga katika nyika ya Sinai.
Wakasafiri kutoka nyika ya Sinai, wakapanga Kibroth-hataava.
Wakasafiri kutoka Kibroth-hataava, wakapanga Haserothi.
Wakasafiri kutoka Haserothi, wakapanga Rithma.
Wakasafiri kutoka Rithma, wakapanga Rimon-peresi.
Wakasafiri kutoka Rimon-peresi, wakapanga Libna.
Wakasafiri kutoka Libna, wakapanga Risa.
Wakasafiri kutoka Risa, wakapanga Keheletha.
Wakasafiri kutoka Keheletha, wakapanga katika mlima wa Sheferi
Wakasafiri kutoka huo mlima wa Sheferi, wakapanga Harada.
Wakasafiri kutoka Harada, wakapanga Makelothi.
Wakasafiri kutoka Tahathi wakapanga Tera.
Wakasafiri kutoka Tera, wakapanga Mithka.
Wakasafiri kutoka Mithka, wakapanga Hashmona.
Wakasafiri kutoka Hashmona, wakapanga Moserothi.
Wakasafiri kutoka Moserothi, wakapanga Bene-yakani.
Wakasafiri kutoka Bene-yakani, wakapanga Hor-hagidgadi.
Wakasafiri kutoka Hor-hagidgadi, wakapanga Yotbatha.
Wakasafiri kutoka Yotbatha, wakapanga Abrona.
Wakasafiri kutoka Abrona, wakapanga Esion-geberi.
Wakasafiri kutoka Esion-geberi, wakapanga katika nyika ya Sini (ni Kadeshi).
Wakasafiri kutoka Kadeshi wakapanga katika mlima wa Hori, katika mpaka wa nchi ya Edomu,
Nao wakasafiri kutoka mlima wa Hori, wakapanga Salmona.
Wakasafiri kutoka Salmona, wakapanga Punoni.
Wakasafiri kutoka Punoni, wakapanga Obothi.
Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika mpaka wa Moabu.
Wakasafiri kutoka Iye-abarimu, wakapanga Dibon-gadi.
Wakasafiri kutoka Dibon-gadi, wakapanga Almon-diblathaimu.
Wakasafiri kutoka Almon-diblathaimu, wakapanga katika milima ya Abarimu, kukabili Nebo.
Wakasafiri kutoka hiyo milima ya Abarimu, wakapanga katika nchi tambarare za Moabu, karibu na mto wa Yordani, hapo Yeriko.
Wakapanga karibu na Yordani, tangu Beth-yeshimothi hata kufikilia Abel-shitimu katika nchi tambarare za Moabu.
Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Libna, na Israeli wote pamoja naye, wakafika Lakishi, wakapanga marago mbele yake na kupigana nao;
Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Lakishi, na Israeli wote pamoja naye, hata wakafikilia Egloni; nao wakapanga marago mbele yake, na kupigana nao;
wakapanga marago juu yao, na kuyaharibu hayo maongeo ya nchi, hata ufikapo Gaza, wala hawakuacha katika Israeli riziki ziwazo zote; kondoo, wala ng'ombe, wala punda.
Kisha akaenda nyikani na kuizunguka hiyo nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu, nao wakapita upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga marago upande wa pili wa Arnoni; wala hawakuingia ndani ya mpaka wa Moabu, kwa maana Arnoni ilikuwa ni mpaka wa Moabu.
Lakini huyo Sihoni hakuwaamini Israeli ili wapite ndani ya mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, nao wakapanga kambi katika Yahasa, wakapigana na Israeli.
Naye Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika, wakatua katika bonde la Ela, nao wakapanga vita juu ya hao Wafilisti.
Wana wa Amoni wakatoka, wakapanga vita mahali pa kuingilia lango; na Washami wa Soba, na wa Rehobu, na watu wa Tobu, na wa Maaka, walikuwa peke yao uwandani.
Akatoka Asa amlaki, wakapanga vita Maresha bondeni mwa Sefatha.