Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani;
Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau.