Nao wote wanaokukimbilia watafurahi; Watapiga daima kelele za furaha. Kwa kuwa Wewe unawahifadhi, Walipendao jina lako watakufurahia.
Wazao wa watumishi wake watairithi, Nao walipendao jina lake watakaa humo.
Unigeukie, unirehemu mimi, Kama iwahusuvyo walipendao jina lako.