Machoni pake mtu asiyefaa hudharauliwa, Bali huwaheshimu wamchao Bwana Ingawa ameapa kwa hasara yake, Hayabadili maneno yake.
Kwako zinatoka sifa zangu Katika kusanyiko kubwa. Nitaziondoa nadhiri zangu Mbele yao wamchao.
Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake.
Tazama, jicho la Bwana li kwao wamchao, Wazingojeao fadhili zake.
Malaika wa Bwana hufanya kituo, Akiwazungukia wamchao na kuwaokoa.
Mcheni Bwana, enyi watakatifu wake, Yaani, wamchao hawahitaji kitu.
Hakika wokovu wake u karibu na wamchao, Utukufu ukae katika nchi yetu.
Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, Kadiri ile ile rehema zake ni kuu kwa wamchao.
Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.
Bali fadhili za Bwana zina wamchao Tangu milele hata milele, Na haki yake ina wana wa wana;
Amewapa wamchao chakula; Atalikumbuka agano lake milele.
Bwana huwaridhia wao wamchao, Na kuzitarajia fadhili zake.
Ajapokuwa mwenye dhambi amefanya maovu mara mia, akazidisha siku zake; lakini hata hivyo najua hakika ya kwamba itakuwa heri kwao wamchao Mungu, wenye kicho mbele zake;