Skip to Content

"wamtafutao"

9 mara katika SUV

Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.

Maana naliona haya kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapanda farasi, ili kutusaidia juu ya adui njiani; kwa maana tulikuwa tumesema na mfalme, tukinena, Mkono wa Mungu u juu ya watu wote wamtafutao, kuwatendea mema; bali uweza wake na ghadhabu yake ni kinyume cha wote wamwachao.

Wapole watakula na kushiba, Wamtafutao Bwana watamsifu; Mioyo yenu na iishi milele.

Hiki ndicho kizazi cha wamtafutao, Wakutafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo.

Wana-simba hutindikiwa, huona njaa; Bali wamtafutao Bwana hawatahitaji kitu cho chote kilicho chema.

Jisifuni kwa jina lake takatifu, Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.

Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.

Watu wabaya hawaelewi na hukumu; Bali wamtafutao Bwana huelewa na yote.

Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.