Skip to Content

"wanawali"

11 mara katika SUV

Naye alikuwa amevaa kanzu ndefu; kwa kuwa kwa nguo hizo huvikwa binti za mfalme waliokuwa wanawali. Ndipo mtumishi wake akamleta nje, akafunga mlango nyuma yake.

Atapelekwa kwa mfalme Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri. Wanawali wenzake wanaomfuata, Watapelekwa kwako.

Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.

Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,

Wako malkia sitini, na masuria themanini, Na wanawali wasiohesabika;

Tahayari, Ee Sidoni; kwa maana bahari imenena, hiyo ngome ya bahari ilisema, Sikuona utungu, wala sikuzaa, wala sikulea vijana, wala sikulea wanawali.

Siku hiyo wanawali wazuri na wavulana watazimia kwa kiu.

Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.

Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.

Kwa habari za wanawali sina amri ya Bwana, lakini natoa shauri langu, mimi niliyejaliwa kwa rehema za Bwana kuwa mwaminifu.