Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake.
Lea alipoona ya kuwa ameacha kuzaa, alimtwaa Zilpa, mjakazi wake, akampa Yakobo kuwa mkewe.
Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya.